Saturday, February 27, 2021

DKT NCHIMBI ATANGAZA NEEMA SINGIDA

MkuuwaMkoa wa Singida Dtk. RehemaNchimbi katikati akiongoza Kongamano
la Fursa za Uwekezaj ikwenye Mkoa wa Singida, Kulia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Singida
Lucy Sheen,
kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi.

Wakuu  waWilaya zaMkoawaSingida(kwenye mstari wa kwanza)
wakifuatilia Mada mbalimbali wakati wa Kongamano la uwekezaji Mkoani Singida.

AfisaUhamasishaji Uwekezaji Mkuu kutoka Kituo cha
Uwekezaji nchini, Joyce Shundu akiwasilisha mada ya
Mazingira na Fursa za Uwekezaji Nchini”amepongeza jitihada na mikakati mbalimbali inayofanywa na MkoawaSingida

Viongozi
wa Wachimbaji Madini Mkoa wa Singida wakiwa kwenye banda lao
wakionyesha madini mbalimbali kwa wadau waliotembelea banda  la wachimbaji wa madini Mkoa wa Singida (SIREMA).


Wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wakionyesha bidhaa zao

  • RAS ASEMA MKOA UMEJIANDAA KIKAMILIFU

 

Na John Mapepele, Singida

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe,
Dkt. Rehema Nchimbi  amewataka  Wawekezaji kutoka  sehemu mbalimbali duniani kuja  kuwekeza 
kwenye  Mkoa wa Singida kwa
kuwa  Mkoa huo umebarikiwa kuwa na  fursa mbalimbali za uwekezaji ambazo bado
hazijatumika kikamilifu.

Akifungua Kongamano la Mwongozo
wa Uwekezaji kwenye Mkoa wa Singida 
kabla ya uzinduzi rasmi wa mwongozo huo, Dkt. Nchimbi amesema  Mkoa wa Singida  ni miongoni mwa  mikoa michache nchini  ambayo 
endapo fursa  zake zikitumika
utachangia  katika maendeleo ya Mkoa na
nchi kwa ujumla

Amezitaja baadhi ya fursa
zilizopo kwenye  Mkoa wa Singida kuwa
ni  pamoja na nishati ya mafuta asilia na
gesi, madini, kilimo cha alizeti,  korosho,utalii,
ufugaji wa nyuki na  kuku pia uwekezaji
kwenye sekta ya michezo ambapo amesema ni zamu ya Mkoa wa Singida  kuchangia 
kikamilifu kwenye uchumi wa nchi. 

Akitoa  mada kuhusu Uwekezaji wa  Alizeti mkoani Singida,
Mratibu wa Utafiti wa Alizeti nchini, Frank  Reuben  amesema zao la alizeti ndiyo zao pekee

linaloweza kuuvusha  mkoa  wa Singida 
kwa kuwa tafiti zinaonyesha kuwa 
mkoa wa Singida  ndiyo unaongoza
hapa nchini kwa  kulima zao hilo.

Ametaja  baadhi ya  maeneo ya fursa za uwekezaji kwenye kilimo cha
Alizeti kuwa ni pamoja na uzalishaji na usambazaji wa mbegu, Kilimo bora
(mesto) cha alizeti na ufugaji nyuki (Agro-apiculture) na uendelezaji wa
viwanda vya kuchakata alizeti, chakula cha mifugo na mazao ya nyuki

Mtafiti wa zao la Korosho, kutoka
Taasisi ya Utafiti wa mazao ya Kilimo (TARI) Dkt. Fortunatus Kapinga  akitoa mada ya zao la Korosho nchini
amesema  Mkoa wa Singida una ardhi nzuri
yenye rutuba ambayo inafaa sana kwa zao la korosho  ukilinganisha na mikoa mingine  hapa nchini hivyo ni fursa pekee kwa  wawekezaji kuja  kufanya uwekezaji katika mkoa huu.

Amezitaja  baadhi ya bidhaa zinazopatikana kwenye zao la
Korosho kuwa ni pamoja na juisi, jamu,mvinyo, maziwa na siagi ambapo amesema
kauli mbiu ya mkoa kwenye uwekezaji kwamba  
“ni zamu yetu” ikitafsiriwa kwa vitendo italeta mageuzi makubwa  katika mkoa wa Singida na taifa kwa ujumla.

Mwenyekiti wanawake wachimbaji
Madini Mkoa wa Singida, Martha  Kayaga
amepongeza Serikali ya awamu ya Tano inayoongizwa  na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa
jitihada kubwa  inayofanya  kuwashilikisha  wachimbaji wazawa kwenye sekta ambapo
ameiomba Serikali kuangalia namna bora ambayo itawawezesha wajimbaji wadogo
wadogo kupata  mitaji hususan  vifaa ili waweze  kuongeza tija katika sekta  hiyo.

Pia Bi. Kayaga ameiomba
Serikali  kuwaangalia wachimbaji wanawake
kwa jicho la pekee kwa kuwa  wao  ni nguzo muhimu kwenye familia na kwamba
asilimia 10 inayotengwa kwenye Halmashauri imekuwa ikielekezwa kwenye sekta nyingine
ambapo amesisitiza endapo itaelekezwa kwa akina mama wachimbaji wadogowadogo
itasaidia kuinua hali za uchumi kuanzia kwenye ngazi ya kaya na Taifa kwa
ujumla.

Kwa upande wake, Afisa  Uhamasishaji Uwekezaji  Mkuu kutoka 
Kituo cha Uwekezaji nchini, Joyce Shundu 
akiwasilisha  mada ya “Mazingira
na Fursa za Uwekezaji Nchini”
  amepongeza 

jitihada na mikakati mbalimbali inayofanywa na Mkoa wa Singida kwa
kwenye uwekezaji  na kutoa wito kwa
wawekezaji kuwahi kuwekeza kwenye  fursa
za kipekee zinazopatikana mkoani hapa.

Awali katika salamu za
utambulisho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi amewataka
Watendaji wote wa Serikali Mkoa wa Singida kuhakikisha wanajituma kufanya kazi
kwa weledi kwenye utoaji huduma  bora kwa
wawekezaji ili azma ya Serikali ya kutaka uwekezaji wenye tija itimie na
maisha  bora kwa watanzania ifikiwe.

Dkt. Lutambi amesema Serikali ya
Mkoa imeshaandaa mazingira wezeshi kwa 
wadau na wawekezaji makini kuja kuwekeza 
kwa kuzingatia sheria  na taratibu
za nchi.

 

 

     MkuuwaMkoa wa Singida Dtk. RehemaNchimbi katikati akiongoza Kongamano
la Fursa za Uwekezaj ikwenye Mkoa wa Singida, Kulia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Singida
Lucy Sheen,
kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi.

Wakuu  waWilaya zaMkoawaSingida(kwenye mstari wa kwanza)
wakifuatilia Mada mbalimbali wakati wa Kongamano la uwekezaji Mkoani Singida.

AfisaUhamasishaji Uwekezaji Mkuu kutoka Kituo cha
Uwekezaji nchini, Joyce Shundu akiwasilisha mada ya
Mazingira na Fursa za Uwekezaji Nchini”amepongeza jitihada na mikakati mbalimbali inayofanywa na MkoawaSingida

1.    

.

Viongozi
wa Wachimbaji Madini Mkoa wa Singida wakiwa kwenye banda lao
wakionyesha madini mbalimbali kwa wadau waliotembelea banda  la wachimbaji wa madini Mkoa wa Singida (SIREMA).


Wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wakionyesha bidhaa zao

  • RAS ASEMA MKOA UMEJIANDAA KIKAMILIFU

 

Na John Mapepele, Singida

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe,
Dkt. Rehema Nchimbi  amewataka  Wawekezaji kutoka  sehemu mbalimbali duniani kuja  kuwekeza 
kwenye  Mkoa wa Singida kwa
kuwa  Mkoa huo umebarikiwa kuwa na  fursa mbalimbali za uwekezaji ambazo bado
hazijatumika kikamilifu.

Akifungua Kongamano la Mwongozo
wa Uwekezaji kwenye Mkoa wa Singida 
kabla ya uzinduzi rasmi wa mwongozo huo, Dkt. Nchimbi amesema  Mkoa wa Singida  ni miongoni mwa  mikoa michache nchini  ambayo 
endapo fursa  zake zikitumika
utachangia  katika maendeleo ya Mkoa na
nchi kwa ujumla

Amezitaja baadhi ya fursa
zilizopo kwenye  Mkoa wa Singida kuwa
ni  pamoja na nishati ya mafuta asilia na
gesi, madini, kilimo cha alizeti,  korosho,utalii,
ufugaji wa nyuki na  kuku pia uwekezaji
kwenye sekta ya michezo ambapo amesema ni zamu ya Mkoa wa Singida  kuchangia 
kikamilifu kwenye uchumi wa nchi. 

Akitoa  mada kuhusu Uwekezaji wa  Alizeti mkoani Singida,
Mratibu wa Utafiti wa Alizeti nchini, Frank  Reuben  amesema zao la alizeti ndiyo zao pekee

linaloweza kuuvusha  mkoa  wa Singida 
kwa kuwa tafiti zinaonyesha kuwa 
mkoa wa Singida  ndiyo unaongoza
hapa nchini kwa  kulima zao hilo.

Ametaja  baadhi ya  maeneo ya fursa za uwekezaji kwenye kilimo cha
Alizeti kuwa ni pamoja na uzalishaji na usambazaji wa mbegu, Kilimo bora
(mesto) cha alizeti na ufugaji nyuki (Agro-apiculture) na uendelezaji wa
viwanda vya kuchakata alizeti, chakula cha mifugo na mazao ya nyuki

Mtafiti wa zao la Korosho, kutoka
Taasisi ya Utafiti wa mazao ya Kilimo (TARI) Dkt. Fortunatus Kapinga  akitoa mada ya zao la Korosho nchini
amesema  Mkoa wa Singida una ardhi nzuri
yenye rutuba ambayo inafaa sana kwa zao la korosho  ukilinganisha na mikoa mingine  hapa nchini hivyo ni fursa pekee kwa  wawekezaji kuja  kufanya uwekezaji katika mkoa huu.

Amezitaja  baadhi ya bidhaa zinazopatikana kwenye zao la
Korosho kuwa ni pamoja na juisi, jamu,mvinyo, maziwa na siagi ambapo amesema
kauli mbiu ya mkoa kwenye uwekezaji kwamba  
“ni zamu yetu” ikitafsiriwa kwa vitendo italeta mageuzi makubwa  katika mkoa wa Singida na taifa kwa ujumla.

Mwenyekiti wanawake wachimbaji
Madini Mkoa wa Singida, Martha  Kayaga
amepongeza Serikali ya awamu ya Tano inayoongizwa  na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa
jitihada kubwa  inayofanya  kuwashilikisha  wachimbaji wazawa kwenye sekta ambapo
ameiomba Serikali kuangalia namna bora ambayo itawawezesha wajimbaji wadogo
wadogo kupata  mitaji hususan  vifaa ili waweze  kuongeza tija katika sekta  hiyo.

Pia Bi. Kayaga ameiomba
Serikali  kuwaangalia wachimbaji wanawake
kwa jicho la pekee kwa kuwa  wao  ni nguzo muhimu kwenye familia na kwamba
asilimia 10 inayotengwa kwenye Halmashauri imekuwa ikielekezwa kwenye sekta nyingine
ambapo amesisitiza endapo itaelekezwa kwa akina mama wachimbaji wadogowadogo
itasaidia kuinua hali za uchumi kuanzia kwenye ngazi ya kaya na Taifa kwa
ujumla.

Kwa upande wake, Afisa  Uhamasishaji Uwekezaji  Mkuu kutoka 
Kituo cha Uwekezaji nchini, Joyce Shundu 
akiwasilisha  mada ya “Mazingira
na Fursa za Uwekezaji Nchini”
  amepongeza 

jitihada na mikakati mbalimbali inayofanywa na Mkoa wa Singida kwa
kwenye uwekezaji  na kutoa wito kwa
wawekezaji kuwahi kuwekeza kwenye  fursa
za kipekee zinazopatikana mkoani hapa.

Awali katika salamu za
utambulisho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi amewataka
Watendaji wote wa Serikali Mkoa wa Singida kuhakikisha wanajituma kufanya kazi
kwa weledi kwenye utoaji huduma  bora kwa
wawekezaji ili azma ya Serikali ya kutaka uwekezaji wenye tija itimie na
maisha  bora kwa watanzania ifikiwe.

Dkt. Lutambi amesema Serikali ya
Mkoa imeshaandaa mazingira wezeshi kwa 
wadau na wawekezaji makini kuja kuwekeza 
kwa kuzingatia sheria  na taratibu
za nchi.

Wednesday, February 17, 2021

AGIZO LA MAGUFULI KUMALIZA MGOGORO WA ARDHI WA BI ELIZABETH MANYONI LATEKELEZWA 100%

 

Bibi Elizabeth Msalali Chilingo (90) (aliyeshika  hati  ya ardhi) akiwa kwenye picha ya pamoja  na  Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi( mwenye msalaba), Viongozi wa  Wilaya ya Manyoni,wataalam wa ardhi  Mkoa  wa Singida na wanafamilia  mara baada ya kukabidhiwa hati hiyo ya eneo lake lilichukuliwa na Afisa Ardhi aitwaye Leonard Msafiri na kisha kupangishwa  kwa Kampuni  mmoja ya simu za mikono ambapo  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliagiza  lirejeshwe mara moja  kwa  bibi huyo ambaye ndiye ataingia  mkataba  wa upangaji na Kampuni  hiyo
Bibi Elizabeth Msalali Chilingo (90) akitoa shukrani zake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  mara baada  ya kukabidhiwa  hati ya eneo lake

                                                          ...........................................................

Na John Mapepele, Manyoni

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi ametekeleza agizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alilomtaka kushirikiana na Viongozi wa Wilaya ya Manyoni kumrejeshea umiliki  wa eneo  lililokuwa mali ya  Bibi Elizabeth Msalali Chilingo (90) ambaye lilichukuliwa na Afisa Ardhi aitwaye Leonard Msafiri na kisha kupangishwa  kwa Kampuni  mmoja ya simu za mikono ambayo  imeweka mnara wa mawasiliano lirejeshwe mara moja  kwa mama huyo ambaye ndiye ataingia  mkataba  wa upangaji na Kampuni  hiyo.

Akikabidhi  hati ya umiliki wa ardhi wa miaka 66 wa eneo hilo la Majengo Kiwanja Na 13 hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Singida  Mhe, Dkt. Rehema Nchimbi amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano  inayoongozwa na Mhe, Dkt. John Pombe  Magufuli ina dhamira ya dhati ya kuwasaidia wananchi wanyonge ili wapate haki zao na kuendelea kufanya shughuli zao za maendeleo ili kuchangia katika uchumi wa kati na hatimaye uchumi wa juu wa Taifa letu.

Amesema Mkoa umejipanga kimkakati kuhakikisha kuwa migogoro yote ya ardhi inakwisha mara moja  kwenye Mkoa wa Singida na kuagiza Wakuu wote wa Wilaya na Wataalam wa ardhi  kuanzia sasa kutatua migogoro ya ardhi katika maeneo husika badala ya kufanya mashauri ya migogoro ya ardhi  maofisini.

“Kuanzia leo sitaki kuona shauri na migogoro ya ardhi ikitatuliwa  maofisini, naagiza wakuu wote wa Wilaya katika Mkoa wangu  na wataalam kwenda moja kwa moja  kutatua  migogoro ya ardhi ya wananchi  katika maeneo ya migogoro, hatua kali zitachukuliwa kwa wote ambao hawatatekeleza  agizo hilo” alisisitiza Mhe. Nchimbi

Akizungumzia kuhusu migogoro ya ardhi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni amesema ni lazima iishe mara moja kwa  kuwa Manyoni  ya sasa ni Sebule ya Makao Makuu ya nchi-Dodoma na kwamba watu kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania wanakuja Manyoni kwa kuwa kuna maeneo mazuri yenye fursa za uwekezaji hususan kwenye  viwanda, biashara  na kilimo cha zao la Korosho ambapo kwa sasa Wilaya hii inaongoza siyo tu Tanzania bali katika  Bara la Afrika kwenye kilimo hicho ambapo kumekuwa na shamba la pamoja la Kilimo cha Korosho (Block Farming)lenye takribani ekari 25000.

“Haiwezekani Manyoni hii ambayo ni lango la makao  makuu ya nchi ikaendelea kuwa na migogoro ya ardhi ambapo sasa  ardhi yake imebeba uwekezaji mkubwa katika nchi yetu” aliongeza Mhe. Mkuu wa Mkoa

 Akipokea hati yake ya umiliki wa eneo hilo, Bibi Elizabeth Msalali  alimshukuru Rais Magufuli kwa kusaidia kupatikana kwa kiwanja chake ambapo amesema Magufuli  ameonyesha kuwa ni Rais anayewapigania  watu masikini na wanyonge kama yeye hivyo anamwombea kwa Mungu azidi kumbariki katika utumishi na maisha yake kwa ujumla.

Aidha Mtoto wa pekee wa Bi Elizabeth ambaye ndiye aliyemwomba Mhe. Rais Magufuli kuingilia kati suala hili Bwana, Adamu Kazimoto alimshukuru na kumpongeza Mkuu wa Mkoa, Dkt. Rehema Nchimbi kwa kuharakisha  kukamilisha  mchakato wa kupata  hati ya umiliki wa kiwanja  hicho kwa mama yake ambapo amesema  mchakato huo umechukua muda mfupi sana.

“Naomba niwe mkweli kama tungekuwa na fedha ya kulipia  hiki kiwanja  nadhani  ingechukua  siku  moja au mbili tu baada ya agizo la Mhe.Rais maana Kamishina Msaidizi wa Mkoa wa Singida Dada Shamimu Hoza alikamilisha  utengenezaji wa hati hiyo mara moja baada ya tamko  hilo la Mhe.Magufuli jambo ambalo limetupa faraja kubwa kwani sasa mama yangu amepata  haki yake” ameongeza Adamu

Akifafanua Adamu amesema suala hili  alianza kufuatilia zaidi ya  miaka tisa iliyopita, na anamshukuru Rais Magufuli  kwa kutoa suluhisho la kudumu ambapo pia ameongeza kwamba mgogoro huo umeifanya familia ya Mzee Kazimoto kuwa kitu kimmoja licha sintofahamu ambazo zilikuwepo hapo awali kwa sababu ya tamaa ya pesa kwa wanafamilia.

Mhe. Rais John Pombe  Magufuli  alilitoa agizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida kushughulikia mgogoro  huo tarehe 31Januari 2021 aliposimama kuwasalimu wananchi wa Manyoni wakati akiwa safarini akitokea Tabora kwenda Dodoma.

Rais Magufuli  alisikiliza  kero inayowakabili wananchi hao ambao walilalamikia  kitendo cha Idara ya Ardhi kuchukua maeneo  yao bila kuwalipa fidia  na wengine kuamriwa  kuondoka katika  eneo hilo baada ya kupewa nyaraka  za kupatiwa  radhi(offer) hali iliyozua mgogoro kati ya wamiliki wa asili wa eneo hilo na Idara ya Ardhi.

Rais ameagiza wananchi wenye offer waruhusiwe kuendeleza maeneo waliyopatiwa na wamiliki wa asili wa eneo hilo  kulipwa fidia kwa mujibu wa Sheria.

Awali, kufuatia agizo  la Mheshimiwa Rais, Timu Maalum ya wataalam kutoka Mkoani na Wilaya ya Manyoni iliyoongozwa na Kamishina Msaidizi wa Mkoa wa Singida Shamimu Hoza Shaban ilikutana  familia nzima ya mmiliki wa asili wa eneo hilo marehemu  Salum Kazimoto aliyefariki mwaka 1973  ambayo   ilikuwa  inavutana  kuhusu  umiliki wa eneo  hilo ambapo  baada ya  majadiliano ilikubaliana kwa kauli mmoja kwamba mmliki halali  wa eneo hilo ni Bibi Elizabeth Msalali.

Kutokana  na  Wilaya ya Manyoni kuonekana kuwa na migogoro ya ardhi kadhaa ya ardhi kwa muda mrefu sasa, mkakati maalum wa kusikiliza kero hizo umeandaliwa  ambapo timu ya wataalam na viongozi wa Halmashauri hiyo unazungukia katika maeneo husika ili kuhakikisha migogoro yote inaisha  kama ilivyoamriwa.

  Na. John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Rufiji. Mhe, Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa wananchi nch...