Saturday, April 16, 2022

 


Na. John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Rufiji. Mhe, Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa wananchi nchini kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye mazoezi ya kitaifa ya uandikishaji wa anuani ya makazi na sensa yanayoendelea hivi sasa nchini kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Mhe, Mchengerwa ameyasema haya leo wakati akiongea na wananchi wa vijiji vya Mgomba, Ngorongo na Kilimani kwenye Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani.

Amefafanua kwamba  mazoezi haya yana faida kubwa kwa nchi yetu  kwa kuwa yanasaidia kupanga  mipango mbalimbali ya maendeleo kwa muda wa sasa  na baadaye.

Aidha, ameishukuru Serikali   ya awamu ya sita kwa kukamilisha mipango ya maendeleo katika kipindi kifupi.


Ametaja baadhi ya mipango ambayo inatekelezwa kuwa ni pamoja na  miundombinu ya barabara, shule na vituo vya afya na jengo la kujifungulia akina mama ambapo amewataka wananchi kutumia na kusimamia vizuri raslimali zinazotolewa.

Aidha ameipongeza Halmashauri ya Rufiji kwa kuwa miongoni mwa Halmashauri inayoongoza kwenye utekelezaji wa mipango ya maendeleo kupitia fedha za ndani.

"Ni jukumu lenu kuhoji kila shilingi ambayo inaletwa lakini pia kushirikiana na Serikali. Na mimi niwaahidi nitaendelea kuipigania Rufiji na mimi ni mtumwa wenu" amesisitiza Mhe. Mchengerwa

Aidha, amewataka wananchi kushirikiana  na Serikali katika kufanya maendeleo na kuendelea kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe,  Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wanyonge.

"Tunamshukuru Mhe. Rais kwa kutujengea Shule ya Sekondari ya Bibi Titi Mohamed ambayo itatoa mchango kwa wananchi wetu". Ameongeza Mhe, Mchengerwa

Katika hatua nyingine Mhe, Mchengerwa Wizara yake inakwenda kuanza kutafuta na kuibua  vipaji vya wachezaji kupitia ligi ya Samia

Friday, January 14, 2022

 Na. John Mapepele- WUSM

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohammed Mchengerwa amesema  Wizara yake itahakikisha inafanya kazi kuanzia ngazi ya mitaa na vijiji  ili kuleta mapinduzi makubwa katika sekta hizo katika kipindi kifupi.

Mhe. Mchengerwa ametoa kauli hiyo usiku wa ( Januari 14, 2022) kuamkia leo akiwa Mgeni Rasmi kwenye fainali za mashindano ya wa sanaa ya Bongo Star Search (BSS) 2022 jijini Dar es Salaam akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wake, Dkt. Hassan Abbasi, na Naibu Katibu Mkuu, Said Yakubu

"Tunataka tuizungumze sanaa katika kila mtaa, tutaizungumza Sanaa katika kila kata, tutaizungumza Sanaa katika kila wilaya, na tutaizungumza Sanaa katika kila mkoa, tunataka Sanaa ndiyo iwe msingi wa kuendeleza katika kulinda na kuendeleza  utamaduni wa taifa letu" amesisitiza Mhe. Mchengerwa

Amesema kwa Wizara yake kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanakwenda  kufanya mageuzi katika sekta ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Aidha,  amesisitiza kuwa yeye ni mtu wa kasi katika utendaji na matokeo zaidi hivyo atahakikisha kuwa  matokeo makubwa yanapatikana katika Wizara yake.

Mhe. Mchengerwa amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara yake. Dkt. Hassan Abbasi kuona uwezekano wa kuwaendeleza washiriki wote wa shindano hilo katika Chuo cha Sanaa Bagamoyo kilicho chini ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Katika mashindano hayo mshindi wa kwanza ni Bryson Yohana kutoka Dar es Salaam ambapo mshindi wa pili ni Andrew Charles kutoka Mwanza na mshindi wa tatu ni Suleiya Abdi mwanadada kutoka mkoa wa Dodoma.



Saturday, December 18, 2021

WAZIRI BASHUNGWA AITAKA MIKOA KUSHIRIKIANA NA WIZARA KUANDAA TUZO ZA FILAMU

 OHN MAPEPELE–WUSM

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Innocent Bashungwa ametoa wito kwa mikoa yote nchini kuiga Mkoa wa Mbeya katika kushirikiana na  Wizara yake  kuandaa Tuzo za Filamu katika miaka ijayo ili kukuza vipaji na kutoa ajira kwa wasanii wengi zaidi walio kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini.

Mhe. Bashungwa ametoa kauli hiyo Jijini Mbeya katika kilele cha utoaji wa Tuzo za Filamu nchini iliyoratibiwa na Bodi ya Filamu chini ya usimamizi wa Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo, Disemba 18, 2021. Mchakato wa kutafuta filamu hizo bora umechukua zaidi ya miezi mitatu.

“Ndugu yangu Comrade Juma Zuberi Homera, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, nakupongeza sana kwa kushirikiana na Bodi ya Filamu chini ya usimamizi wa wizara yangu.”amesisitiza Mhe. Bashungwa

Mhe. Bashungwa amesema kufanyika kwa tamasha hili la kwanza katika historia ya Tanzania kabla na baada ya  uhuru ni utekelezaji wa  azma ya Serikali ya kushirikisha wadau, kurejesha utamaduni wa kutoa tuzo kwa wadau wa sekta za Utamaduni, Sanaa na Michezo hapa nchini.

Aidha amesema Serikali imeshatenga  kiasi cha bilioni 1.5 kwenye mfuko wa Maendeleo ya Sanaa na Utamaduni kwa ajili kukuza na kuendeleza  shughuli za Utamaduni na Sanaa ikiwa ni pamoja na Filamu.

“Ninawajulisha kuwa tuzo hizi ni endelevu, hivyo ninawakaribisha wadau wote wenye nia ya kushirikiana na Serikali kwa mwaka 2022.” Amehimiza Mhe. Bashungwa.

Pia aliipongeza Bodi ya Filamu kwa ubunifu huu ambao umeonesha dira ya Serikali katika kukuza na kuendeleza sekta ya sanaa nchini.

Waziri Bashungwa ameongeza kutokana na umuhimu na mapenzi yake kwenye tasnia ya filamu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan pamoja na majukumu mengi aliyonayo ameandaa filamu ya Royal Tour ambayo inalenga kuchochea maendeleo ya nchi yetu kwa kuitangaza taswira ya Tanzania na kuvutia watalii na wawekezaji nchini.

Katika Kilele hicho Rais Samia Suluhu Hassan amepewa tuzo ya heshima kwa mchango wake katika tasnia ya filamu nchini tuzo hiyo ilipokelewa kwa niaba yake na Mhe. Innocent Bashungwa huku Mhe. Bashungwa na Naibu wake Bi Pauline Gekul wakipokea tuzo  na wasanii 30 kunyakua tuzo za filamu nchini.

Hafla ya kilele cha Tuzo za Filamu nchini imehudhuriwa na viongozi kadhaa wa serikali akiwamo Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Dkt.Tulia Akson ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Zuberi Homera, Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Dkt, Hassan Abbasi,Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Dkt. Angelina Lutambi na viongozi kadhaa wa mikoa ya Mbeya na mikoa jirani, na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Injinia Maryprisca Mahundi.






Friday, December 10, 2021

Vyama Vya Michezo Tumieni Taifa CUP Kuwapata Wachezaji Bora Wa Taifa- Bashungwa

 Na John Mapepele.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Innocent l. Bashungwa ametoa wito kwa vyama vya kitaifa vya michezo, kutumia mashindano ya Taifa CUP 2021 kuchagua vipaji vya wachezaji na kuviendeleza ili kupata vipaji vitakavyounda timu za Taifa za michezo mbalimbali kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.

Mhe. Bashungwa ameyasema hayo, leo Desemba 10,2021 wakati alipokuwa akifungua mashindano ya Taifa CUP 2021 kwenye Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.

 Amesema azma ya Serikali ni kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania, wanashiriki kikamilifu katika shughuli za michezo kwa kuwa michezo inatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi hususan kwenye Marnie ya uchumi, siasa na jamii.

“Kimsingi michezo ni ajira, amani, mshikamano, afya na furaha. Kutokana na umuhimu huu wa sekta ya michezo, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imeamua kwa dhati kabisa, kwa kusaidiana na Vyama vya Michezo chini ya Baraza la Michezo la Taifa, kuanzisha shindano la Taifa Cup ambalo lilikuwa halipo kwa miaka kadhaa”. Amefafanua Mhe. Bashungwa.

Amesema, mashindano ya Taifa Cup 2021 yameshirikisha michezo michezo mitatu ambayo ni soka, netiboli na riadha pamoja na michezo ya jadi.

Ameongeza kuwa amefarijika kuona wananchi wa pande mbili za Muungano wameendelea kuunganishwa   na mashindano haya na wanashirikiana vyema, kupitia sekta  ya michezo, ambapo amesisitiza kuwa ana amini kuwa katika mashindano haya, kutakuwa ushindani mkubwa katika michezo yote mitatu, na aliyejiandaa vema ndie atakaye kuwa mshindi

Kupitia hotuba yake amemshukuru Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa dhamira yake ya dhati ya kutaka kuona sekta ya michezo, pamoja na sekta za Utamaduni na Sanaa, zinapiga hatua kubwa kwa manufaa ya Watanzania.Amepongeza kamati ya maandalizi ya mashindano haya na viongozi wa mikoa yote iliyoleta timu zao kwenye mashindano haya, bila kujali changamoto mbalimbali katika kuandaa ikiwa ni pamoja na maandalizi ya timu, na kuzisafirisha mpaka hapa Dar es Salaam.

Ametoa rai kwa wanamichezo wanaoshiriki mashindano hayoambao bado hawajachanja, kwenda kuchanja ili kujikinga na ugonjwa wa Uviko 19 na amewakumbusha watanzania wote kuchukuwa hatua za kujikinga na maambukizi ya virusi vya korona, kwa kuwa ugonjwa huo bado upo ambapo amesisitiza kuwa ni wajibu wa kila mwananchi kunachukua hatua madhubuti, kadiri ya maelekezo ya wataalamu wetu wa afya.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Innocent l. Bashungwa

Saturday, February 27, 2021

DKT NCHIMBI ATANGAZA NEEMA SINGIDA

MkuuwaMkoa wa Singida Dtk. RehemaNchimbi katikati akiongoza Kongamano
la Fursa za Uwekezaj ikwenye Mkoa wa Singida, Kulia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Singida
Lucy Sheen,
kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi.

Wakuu  waWilaya zaMkoawaSingida(kwenye mstari wa kwanza)
wakifuatilia Mada mbalimbali wakati wa Kongamano la uwekezaji Mkoani Singida.

AfisaUhamasishaji Uwekezaji Mkuu kutoka Kituo cha
Uwekezaji nchini, Joyce Shundu akiwasilisha mada ya
Mazingira na Fursa za Uwekezaji Nchini”amepongeza jitihada na mikakati mbalimbali inayofanywa na MkoawaSingida

Viongozi
wa Wachimbaji Madini Mkoa wa Singida wakiwa kwenye banda lao
wakionyesha madini mbalimbali kwa wadau waliotembelea banda  la wachimbaji wa madini Mkoa wa Singida (SIREMA).


Wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wakionyesha bidhaa zao

  • RAS ASEMA MKOA UMEJIANDAA KIKAMILIFU

 

Na John Mapepele, Singida

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe,
Dkt. Rehema Nchimbi  amewataka  Wawekezaji kutoka  sehemu mbalimbali duniani kuja  kuwekeza 
kwenye  Mkoa wa Singida kwa
kuwa  Mkoa huo umebarikiwa kuwa na  fursa mbalimbali za uwekezaji ambazo bado
hazijatumika kikamilifu.

Akifungua Kongamano la Mwongozo
wa Uwekezaji kwenye Mkoa wa Singida 
kabla ya uzinduzi rasmi wa mwongozo huo, Dkt. Nchimbi amesema  Mkoa wa Singida  ni miongoni mwa  mikoa michache nchini  ambayo 
endapo fursa  zake zikitumika
utachangia  katika maendeleo ya Mkoa na
nchi kwa ujumla

Amezitaja baadhi ya fursa
zilizopo kwenye  Mkoa wa Singida kuwa
ni  pamoja na nishati ya mafuta asilia na
gesi, madini, kilimo cha alizeti,  korosho,utalii,
ufugaji wa nyuki na  kuku pia uwekezaji
kwenye sekta ya michezo ambapo amesema ni zamu ya Mkoa wa Singida  kuchangia 
kikamilifu kwenye uchumi wa nchi. 

Akitoa  mada kuhusu Uwekezaji wa  Alizeti mkoani Singida,
Mratibu wa Utafiti wa Alizeti nchini, Frank  Reuben  amesema zao la alizeti ndiyo zao pekee

linaloweza kuuvusha  mkoa  wa Singida 
kwa kuwa tafiti zinaonyesha kuwa 
mkoa wa Singida  ndiyo unaongoza
hapa nchini kwa  kulima zao hilo.

Ametaja  baadhi ya  maeneo ya fursa za uwekezaji kwenye kilimo cha
Alizeti kuwa ni pamoja na uzalishaji na usambazaji wa mbegu, Kilimo bora
(mesto) cha alizeti na ufugaji nyuki (Agro-apiculture) na uendelezaji wa
viwanda vya kuchakata alizeti, chakula cha mifugo na mazao ya nyuki

Mtafiti wa zao la Korosho, kutoka
Taasisi ya Utafiti wa mazao ya Kilimo (TARI) Dkt. Fortunatus Kapinga  akitoa mada ya zao la Korosho nchini
amesema  Mkoa wa Singida una ardhi nzuri
yenye rutuba ambayo inafaa sana kwa zao la korosho  ukilinganisha na mikoa mingine  hapa nchini hivyo ni fursa pekee kwa  wawekezaji kuja  kufanya uwekezaji katika mkoa huu.

Amezitaja  baadhi ya bidhaa zinazopatikana kwenye zao la
Korosho kuwa ni pamoja na juisi, jamu,mvinyo, maziwa na siagi ambapo amesema
kauli mbiu ya mkoa kwenye uwekezaji kwamba  
“ni zamu yetu” ikitafsiriwa kwa vitendo italeta mageuzi makubwa  katika mkoa wa Singida na taifa kwa ujumla.

Mwenyekiti wanawake wachimbaji
Madini Mkoa wa Singida, Martha  Kayaga
amepongeza Serikali ya awamu ya Tano inayoongizwa  na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa
jitihada kubwa  inayofanya  kuwashilikisha  wachimbaji wazawa kwenye sekta ambapo
ameiomba Serikali kuangalia namna bora ambayo itawawezesha wajimbaji wadogo
wadogo kupata  mitaji hususan  vifaa ili waweze  kuongeza tija katika sekta  hiyo.

Pia Bi. Kayaga ameiomba
Serikali  kuwaangalia wachimbaji wanawake
kwa jicho la pekee kwa kuwa  wao  ni nguzo muhimu kwenye familia na kwamba
asilimia 10 inayotengwa kwenye Halmashauri imekuwa ikielekezwa kwenye sekta nyingine
ambapo amesisitiza endapo itaelekezwa kwa akina mama wachimbaji wadogowadogo
itasaidia kuinua hali za uchumi kuanzia kwenye ngazi ya kaya na Taifa kwa
ujumla.

Kwa upande wake, Afisa  Uhamasishaji Uwekezaji  Mkuu kutoka 
Kituo cha Uwekezaji nchini, Joyce Shundu 
akiwasilisha  mada ya “Mazingira
na Fursa za Uwekezaji Nchini”
  amepongeza 

jitihada na mikakati mbalimbali inayofanywa na Mkoa wa Singida kwa
kwenye uwekezaji  na kutoa wito kwa
wawekezaji kuwahi kuwekeza kwenye  fursa
za kipekee zinazopatikana mkoani hapa.

Awali katika salamu za
utambulisho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi amewataka
Watendaji wote wa Serikali Mkoa wa Singida kuhakikisha wanajituma kufanya kazi
kwa weledi kwenye utoaji huduma  bora kwa
wawekezaji ili azma ya Serikali ya kutaka uwekezaji wenye tija itimie na
maisha  bora kwa watanzania ifikiwe.

Dkt. Lutambi amesema Serikali ya
Mkoa imeshaandaa mazingira wezeshi kwa 
wadau na wawekezaji makini kuja kuwekeza 
kwa kuzingatia sheria  na taratibu
za nchi.

 

 

     MkuuwaMkoa wa Singida Dtk. RehemaNchimbi katikati akiongoza Kongamano
la Fursa za Uwekezaj ikwenye Mkoa wa Singida, Kulia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Singida
Lucy Sheen,
kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi.

Wakuu  waWilaya zaMkoawaSingida(kwenye mstari wa kwanza)
wakifuatilia Mada mbalimbali wakati wa Kongamano la uwekezaji Mkoani Singida.

AfisaUhamasishaji Uwekezaji Mkuu kutoka Kituo cha
Uwekezaji nchini, Joyce Shundu akiwasilisha mada ya
Mazingira na Fursa za Uwekezaji Nchini”amepongeza jitihada na mikakati mbalimbali inayofanywa na MkoawaSingida

1.    

.

Viongozi
wa Wachimbaji Madini Mkoa wa Singida wakiwa kwenye banda lao
wakionyesha madini mbalimbali kwa wadau waliotembelea banda  la wachimbaji wa madini Mkoa wa Singida (SIREMA).


Wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wakionyesha bidhaa zao

  • RAS ASEMA MKOA UMEJIANDAA KIKAMILIFU

 

Na John Mapepele, Singida

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe,
Dkt. Rehema Nchimbi  amewataka  Wawekezaji kutoka  sehemu mbalimbali duniani kuja  kuwekeza 
kwenye  Mkoa wa Singida kwa
kuwa  Mkoa huo umebarikiwa kuwa na  fursa mbalimbali za uwekezaji ambazo bado
hazijatumika kikamilifu.

Akifungua Kongamano la Mwongozo
wa Uwekezaji kwenye Mkoa wa Singida 
kabla ya uzinduzi rasmi wa mwongozo huo, Dkt. Nchimbi amesema  Mkoa wa Singida  ni miongoni mwa  mikoa michache nchini  ambayo 
endapo fursa  zake zikitumika
utachangia  katika maendeleo ya Mkoa na
nchi kwa ujumla

Amezitaja baadhi ya fursa
zilizopo kwenye  Mkoa wa Singida kuwa
ni  pamoja na nishati ya mafuta asilia na
gesi, madini, kilimo cha alizeti,  korosho,utalii,
ufugaji wa nyuki na  kuku pia uwekezaji
kwenye sekta ya michezo ambapo amesema ni zamu ya Mkoa wa Singida  kuchangia 
kikamilifu kwenye uchumi wa nchi. 

Akitoa  mada kuhusu Uwekezaji wa  Alizeti mkoani Singida,
Mratibu wa Utafiti wa Alizeti nchini, Frank  Reuben  amesema zao la alizeti ndiyo zao pekee

linaloweza kuuvusha  mkoa  wa Singida 
kwa kuwa tafiti zinaonyesha kuwa 
mkoa wa Singida  ndiyo unaongoza
hapa nchini kwa  kulima zao hilo.

Ametaja  baadhi ya  maeneo ya fursa za uwekezaji kwenye kilimo cha
Alizeti kuwa ni pamoja na uzalishaji na usambazaji wa mbegu, Kilimo bora
(mesto) cha alizeti na ufugaji nyuki (Agro-apiculture) na uendelezaji wa
viwanda vya kuchakata alizeti, chakula cha mifugo na mazao ya nyuki

Mtafiti wa zao la Korosho, kutoka
Taasisi ya Utafiti wa mazao ya Kilimo (TARI) Dkt. Fortunatus Kapinga  akitoa mada ya zao la Korosho nchini
amesema  Mkoa wa Singida una ardhi nzuri
yenye rutuba ambayo inafaa sana kwa zao la korosho  ukilinganisha na mikoa mingine  hapa nchini hivyo ni fursa pekee kwa  wawekezaji kuja  kufanya uwekezaji katika mkoa huu.

Amezitaja  baadhi ya bidhaa zinazopatikana kwenye zao la
Korosho kuwa ni pamoja na juisi, jamu,mvinyo, maziwa na siagi ambapo amesema
kauli mbiu ya mkoa kwenye uwekezaji kwamba  
“ni zamu yetu” ikitafsiriwa kwa vitendo italeta mageuzi makubwa  katika mkoa wa Singida na taifa kwa ujumla.

Mwenyekiti wanawake wachimbaji
Madini Mkoa wa Singida, Martha  Kayaga
amepongeza Serikali ya awamu ya Tano inayoongizwa  na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa
jitihada kubwa  inayofanya  kuwashilikisha  wachimbaji wazawa kwenye sekta ambapo
ameiomba Serikali kuangalia namna bora ambayo itawawezesha wajimbaji wadogo
wadogo kupata  mitaji hususan  vifaa ili waweze  kuongeza tija katika sekta  hiyo.

Pia Bi. Kayaga ameiomba
Serikali  kuwaangalia wachimbaji wanawake
kwa jicho la pekee kwa kuwa  wao  ni nguzo muhimu kwenye familia na kwamba
asilimia 10 inayotengwa kwenye Halmashauri imekuwa ikielekezwa kwenye sekta nyingine
ambapo amesisitiza endapo itaelekezwa kwa akina mama wachimbaji wadogowadogo
itasaidia kuinua hali za uchumi kuanzia kwenye ngazi ya kaya na Taifa kwa
ujumla.

Kwa upande wake, Afisa  Uhamasishaji Uwekezaji  Mkuu kutoka 
Kituo cha Uwekezaji nchini, Joyce Shundu 
akiwasilisha  mada ya “Mazingira
na Fursa za Uwekezaji Nchini”
  amepongeza 

jitihada na mikakati mbalimbali inayofanywa na Mkoa wa Singida kwa
kwenye uwekezaji  na kutoa wito kwa
wawekezaji kuwahi kuwekeza kwenye  fursa
za kipekee zinazopatikana mkoani hapa.

Awali katika salamu za
utambulisho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi amewataka
Watendaji wote wa Serikali Mkoa wa Singida kuhakikisha wanajituma kufanya kazi
kwa weledi kwenye utoaji huduma  bora kwa
wawekezaji ili azma ya Serikali ya kutaka uwekezaji wenye tija itimie na
maisha  bora kwa watanzania ifikiwe.

Dkt. Lutambi amesema Serikali ya
Mkoa imeshaandaa mazingira wezeshi kwa 
wadau na wawekezaji makini kuja kuwekeza 
kwa kuzingatia sheria  na taratibu
za nchi.

Wednesday, February 17, 2021

AGIZO LA MAGUFULI KUMALIZA MGOGORO WA ARDHI WA BI ELIZABETH MANYONI LATEKELEZWA 100%

 

Bibi Elizabeth Msalali Chilingo (90) (aliyeshika  hati  ya ardhi) akiwa kwenye picha ya pamoja  na  Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi( mwenye msalaba), Viongozi wa  Wilaya ya Manyoni,wataalam wa ardhi  Mkoa  wa Singida na wanafamilia  mara baada ya kukabidhiwa hati hiyo ya eneo lake lilichukuliwa na Afisa Ardhi aitwaye Leonard Msafiri na kisha kupangishwa  kwa Kampuni  mmoja ya simu za mikono ambapo  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliagiza  lirejeshwe mara moja  kwa  bibi huyo ambaye ndiye ataingia  mkataba  wa upangaji na Kampuni  hiyo
Bibi Elizabeth Msalali Chilingo (90) akitoa shukrani zake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  mara baada  ya kukabidhiwa  hati ya eneo lake

                                                          ...........................................................

Na John Mapepele, Manyoni

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi ametekeleza agizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alilomtaka kushirikiana na Viongozi wa Wilaya ya Manyoni kumrejeshea umiliki  wa eneo  lililokuwa mali ya  Bibi Elizabeth Msalali Chilingo (90) ambaye lilichukuliwa na Afisa Ardhi aitwaye Leonard Msafiri na kisha kupangishwa  kwa Kampuni  mmoja ya simu za mikono ambayo  imeweka mnara wa mawasiliano lirejeshwe mara moja  kwa mama huyo ambaye ndiye ataingia  mkataba  wa upangaji na Kampuni  hiyo.

Akikabidhi  hati ya umiliki wa ardhi wa miaka 66 wa eneo hilo la Majengo Kiwanja Na 13 hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Singida  Mhe, Dkt. Rehema Nchimbi amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano  inayoongozwa na Mhe, Dkt. John Pombe  Magufuli ina dhamira ya dhati ya kuwasaidia wananchi wanyonge ili wapate haki zao na kuendelea kufanya shughuli zao za maendeleo ili kuchangia katika uchumi wa kati na hatimaye uchumi wa juu wa Taifa letu.

Amesema Mkoa umejipanga kimkakati kuhakikisha kuwa migogoro yote ya ardhi inakwisha mara moja  kwenye Mkoa wa Singida na kuagiza Wakuu wote wa Wilaya na Wataalam wa ardhi  kuanzia sasa kutatua migogoro ya ardhi katika maeneo husika badala ya kufanya mashauri ya migogoro ya ardhi  maofisini.

“Kuanzia leo sitaki kuona shauri na migogoro ya ardhi ikitatuliwa  maofisini, naagiza wakuu wote wa Wilaya katika Mkoa wangu  na wataalam kwenda moja kwa moja  kutatua  migogoro ya ardhi ya wananchi  katika maeneo ya migogoro, hatua kali zitachukuliwa kwa wote ambao hawatatekeleza  agizo hilo” alisisitiza Mhe. Nchimbi

Akizungumzia kuhusu migogoro ya ardhi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni amesema ni lazima iishe mara moja kwa  kuwa Manyoni  ya sasa ni Sebule ya Makao Makuu ya nchi-Dodoma na kwamba watu kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania wanakuja Manyoni kwa kuwa kuna maeneo mazuri yenye fursa za uwekezaji hususan kwenye  viwanda, biashara  na kilimo cha zao la Korosho ambapo kwa sasa Wilaya hii inaongoza siyo tu Tanzania bali katika  Bara la Afrika kwenye kilimo hicho ambapo kumekuwa na shamba la pamoja la Kilimo cha Korosho (Block Farming)lenye takribani ekari 25000.

“Haiwezekani Manyoni hii ambayo ni lango la makao  makuu ya nchi ikaendelea kuwa na migogoro ya ardhi ambapo sasa  ardhi yake imebeba uwekezaji mkubwa katika nchi yetu” aliongeza Mhe. Mkuu wa Mkoa

 Akipokea hati yake ya umiliki wa eneo hilo, Bibi Elizabeth Msalali  alimshukuru Rais Magufuli kwa kusaidia kupatikana kwa kiwanja chake ambapo amesema Magufuli  ameonyesha kuwa ni Rais anayewapigania  watu masikini na wanyonge kama yeye hivyo anamwombea kwa Mungu azidi kumbariki katika utumishi na maisha yake kwa ujumla.

Aidha Mtoto wa pekee wa Bi Elizabeth ambaye ndiye aliyemwomba Mhe. Rais Magufuli kuingilia kati suala hili Bwana, Adamu Kazimoto alimshukuru na kumpongeza Mkuu wa Mkoa, Dkt. Rehema Nchimbi kwa kuharakisha  kukamilisha  mchakato wa kupata  hati ya umiliki wa kiwanja  hicho kwa mama yake ambapo amesema  mchakato huo umechukua muda mfupi sana.

“Naomba niwe mkweli kama tungekuwa na fedha ya kulipia  hiki kiwanja  nadhani  ingechukua  siku  moja au mbili tu baada ya agizo la Mhe.Rais maana Kamishina Msaidizi wa Mkoa wa Singida Dada Shamimu Hoza alikamilisha  utengenezaji wa hati hiyo mara moja baada ya tamko  hilo la Mhe.Magufuli jambo ambalo limetupa faraja kubwa kwani sasa mama yangu amepata  haki yake” ameongeza Adamu

Akifafanua Adamu amesema suala hili  alianza kufuatilia zaidi ya  miaka tisa iliyopita, na anamshukuru Rais Magufuli  kwa kutoa suluhisho la kudumu ambapo pia ameongeza kwamba mgogoro huo umeifanya familia ya Mzee Kazimoto kuwa kitu kimmoja licha sintofahamu ambazo zilikuwepo hapo awali kwa sababu ya tamaa ya pesa kwa wanafamilia.

Mhe. Rais John Pombe  Magufuli  alilitoa agizo kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida kushughulikia mgogoro  huo tarehe 31Januari 2021 aliposimama kuwasalimu wananchi wa Manyoni wakati akiwa safarini akitokea Tabora kwenda Dodoma.

Rais Magufuli  alisikiliza  kero inayowakabili wananchi hao ambao walilalamikia  kitendo cha Idara ya Ardhi kuchukua maeneo  yao bila kuwalipa fidia  na wengine kuamriwa  kuondoka katika  eneo hilo baada ya kupewa nyaraka  za kupatiwa  radhi(offer) hali iliyozua mgogoro kati ya wamiliki wa asili wa eneo hilo na Idara ya Ardhi.

Rais ameagiza wananchi wenye offer waruhusiwe kuendeleza maeneo waliyopatiwa na wamiliki wa asili wa eneo hilo  kulipwa fidia kwa mujibu wa Sheria.

Awali, kufuatia agizo  la Mheshimiwa Rais, Timu Maalum ya wataalam kutoka Mkoani na Wilaya ya Manyoni iliyoongozwa na Kamishina Msaidizi wa Mkoa wa Singida Shamimu Hoza Shaban ilikutana  familia nzima ya mmiliki wa asili wa eneo hilo marehemu  Salum Kazimoto aliyefariki mwaka 1973  ambayo   ilikuwa  inavutana  kuhusu  umiliki wa eneo  hilo ambapo  baada ya  majadiliano ilikubaliana kwa kauli mmoja kwamba mmliki halali  wa eneo hilo ni Bibi Elizabeth Msalali.

Kutokana  na  Wilaya ya Manyoni kuonekana kuwa na migogoro ya ardhi kadhaa ya ardhi kwa muda mrefu sasa, mkakati maalum wa kusikiliza kero hizo umeandaliwa  ambapo timu ya wataalam na viongozi wa Halmashauri hiyo unazungukia katika maeneo husika ili kuhakikisha migogoro yote inaisha  kama ilivyoamriwa.

  Na. John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Rufiji. Mhe, Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa wananchi nch...